Sunday, October 4, 2015
TABIA YA WATU WASIO NA MAFANIKIO
1. Ni watu wenye tabia ya kujipendelea wao wenyewe, watu wenye umimi na ubinafsi wakati wote
2. Ni watu wenye tabia ya ubishi na kupinga kila jambo, hususani lile ambalo mwingine amelisema ama kulizungumza, kwao hoja ya mwingine sio hoja bali hoja yao ndiyo hoja pekee.
3. Ni watu wenye visasi na mafundo ya moyoni hata katika vitu vidogo na visivyo vya msingi, wanaweza kuzira kirahisi tena kwa muda mrefu bila hata sababu ya msingi
4. Wanaumizwa sana pale mwingine anapopewa pongezi au kusifiwa au kupewa ushindi, kiu yao ni kwamba pongezi zote na sifa zote na ushindi wote uwe wakwao. Mara mwingine anapoonekana kushinda basi wao hujifanya ndio waliokuwa chachu au wasababishaji wa ushindi huo na kwahivyo wanataka wapongezwe wao au mchango wao kukubalika mbele za watu
5. Ni watu walalamishi sana na wenye kulaumu kila mazingira, huwalaumu wengine pale wao wanapoonekana kushindwa, wakishindwa au kufeli wao basi huzitupia lawama kwa watu wanaowazunguka, utasikia wakisema “kama asingekuwa fulani basi nisingeshindwa hivi, yeye ndiyo amesababisha mimi kufeli au kutofanya vizuri”
6. Wanapenda na wala hawaoni tatizo kupoteza muda, anaweza kukaa mbele ya televisheni masaa na masaaa bila kujali muda unavyopotea
7. Mara nyingine hujaribu kujiwekea mpangilio wa siku wa nini atafanya na wakati gani lakini kamwe hawawezi kufwata walichokipanga wenyewe
8. Ni waoga na wapinzani wa mabadiliko hata kama hawanauhakika nini asili ya mabadiliko hayo
9. Mara zote hudhani na hufikiri kuwa wanajua kila kitu, ni ngumu sana kuishi na mtu wa aina hii kwa maana wakati wote ni ngumu kumbadili au kubadili lile analoliwaza au kulifikiri maana yeye anauhakika kuwa anafahamu kuliko mwingine yeyote
10. Katika kila wanalofanya wao husukumwa na mawazo au kiu ya kujua nini anafaidika nacho, kama yeye hapati manufaa ya moja kwa moja katika chochote afanyacho basi hawezi kushiriki chochote. Watu wahivi ni ngumu sana kusaidia mtu mwingine au kutoa mchango wa hali na mali kwa jamii maana wao huona kuwa hauna faida za moja kwa moja kwake.
11. Ni watu wanaopenda kuwazungumzia wengine, huzungumzia madhaifu ya watu na kushindwa kwa wengine, hata siku moja hawawezi kujadili mafanikio ya mtu mwingine
12. Mara nyingi ndani ya mioyo yao huwaza au kutamani wengine washindwe au wasiendelee, tena sio kutamani tu bali huumia wanapoona wengine wanafanikiwa
13. Sio wepesi wa kutoa taarifa muhimu kwa wengine, ni wafichaji wa taarifa za muhimu maana ndani yao wanakiu ya kuzuia maendeleo yaw engine au kuona wengine wanafanikiwa
14. Hawafahamu wala hawajui nini wanatamani wala ni nini wanataka maishani, kwa maana hiyo ni ngumu kufikia katika mustakabali wowote
15. Ni watu wenye hasira au kushindwa kujizuia kuonyesha hasira zao
16. Ni watu wasio na malengo, wasioweka malengo binafsi na wala hawawezi kuyafuata malengo yao, kwa hali hiyo basi inakuwa ngumu kufikia mafanikio maishani mwao.
Saturday, October 3, 2015
TABIA ZA WATU WALIO FANIKIWA
Kufanikiwa ni kiu ya kila mmoja ingawa ukweli ni kwamba wengi wetu tunabaki tunayatamani mafanikio wakati hatuna mazingira yeyote ya kuruhusu mafanikio hayo yawepo au yatujie. Hapa nakuletea tabia za watu wawili tofauti, mmoja akiwa ni mtu mwenye mafanikio au yule ambaye ana mazingira ya kuja kufanikiwa na mwingine ni mtu asiye na mafanikio na asiye na mazingira ya kufanikiwa maishani. Nitaanza na tabia za watu wenye mafanikio;
1. Ni watu wenye kushukuru kwa kila jambo, sio wenye kutoa lawama
2. Ni watu wenye tabia ya kupongeza pale wanapoona mwingine anastahili pongezi
3. Ni watu wenye tabia ya kusamehe, tena wanasamehe kwa urahisi wala sio kwa kuombwa na kulazimishwa
4. Ni watu wasioona uchungu kuwapongeza wengine au kukubali wengine wanapopata ushindi wa aina yeyote, na sio tu kuwapongeza bali pia hawaoni ugumu kuwasaidia au kuwashauri wengine ili wafanikiwe zaidi
5. Ni watu wanaokubali wakati wote kubeba majukumu au lawama pale wanaposhindwa kufanya inavyopaswa, sio wenye kujitetea au kujaribu kukwepa majukumu
6. Ni watu wenye tabia ya kupenda kusoma kitu kila siku, sio wavivu wa kusoma au kutafuta taarifa na ujuzi
7. Ni watu wenye tabia ya kuweka utaratibu wa nini kinafanyila leo na nini kitafanyika kesho na kwa nini kifanyike, sio watu wanaoburuzwa na mazingira yanaowazunguka au kuendeshwa na marafiki zao
8. Sio watu wenye kuzungumza sana kuhusu watu wengine na madhaifu yaw engine bali ni wenye kuzungumza zaidi kuhusu mawazo ya kujenga au mawazo ya kimaendeleo
9. Mara zote wana kiu ya kuona wengine wanafanikiwa, hata kama mafanikio hayo yatayazidi yale wao walionayo
10. Sio wachoyo katika kutoa taarifa au ujumbe wowote muhimu kwa mtu yeyote, maana wao hawana uchungu na mafanikio au ushindi wa mwingine
11. Ni watu wenye kuonyesha furaha wakati wote, sio wenye kununa, kuzira na kuwa na huzuni mara kwa mara
12. Ni watu wanaoweka malengo na kuongozwa na malengo katika maisha yao ya kila siku, sio wanaokurupuka kufanya mambo kwa hisia, misukumo au mashindano tu
13. Sio waoga wa mabadiliko, bali hutamani mabadiliko chanya na yenye kujenga na kuleta maendeleo, na kwahiyo mara zote kuyawezesha mabadiliko kutokea kwao na kwenye maisha ya wengine na sio kuyapinga
14. Kwao kujifunza ni tabia endelevu sio jambo linalotokea wakati wakiwa shuleni tu, wao huhesabu maisha ya kila siku ni kama shule
15. Kiu na msukumo wa maisha yao ya kila siku ni katika kusababisha mabadiliko, aidha mabadiliko kwao wao binafsi au kwa wale wanaowazunguka.
ILI UFANIKIWE UNAHITAJI UWE NA TABIA HIZi
Kufanikiwa ni kiu ya kila mmoja ingawa ukweli ni kwamba wengi wetu tunabaki tunayatamani mafanikio wakati hatuna mazingira yeyote ya kuruhusu mafanikio hayo yawepo au yatujie. Hapa nakuletea tabia za watu wawili tofauti, mmoja akiwa ni mtu mwenye mafanikio au yule ambaye ana mazingira ya kuja kufanikiwa na mwingine ni mtu asiye na mafanikio na asiye na mazingira ya kufanikiwa maishani. Nitaanza na tabia za watu wenye mafanikio;
1. Ni watu wenye kushukuru kwa kila jambo, sio wenye kutoa lawama
2. Ni watu wenye tabia ya kupongeza pale wanapoona mwingine anastahili pongezi
3. Ni watu wenye tabia ya kusamehe, tena wanasamehe kwa urahisi wala sio kwa kuombwa na kulazimishwa
4. Ni watu wasioona uchungu kuwapongeza wengine au kukubali wengine wanapopata ushindi wa aina yeyote, na sio tu kuwapongeza bali pia hawaoni ugumu kuwasaidia au kuwashauri wengine ili wafanikiwe zaidi
5. Ni watu wanaokubali wakati wote kubeba majukumu au lawama pale wanaposhindwa kufanya inavyopaswa, sio wenye kujitetea au kujaribu kukwepa majukumu
6. Ni watu wenye tabia ya kupenda kusoma kitu kila siku, sio wavivu wa kusoma au kutafuta taarifa na ujuzi
7. Ni watu wenye tabia ya kuweka utaratibu wa nini kinafanyila leo na nini kitafanyika kesho na kwa nini kifanyike, sio watu wanaoburuzwa na mazingira yanaowazunguka au kuendeshwa na marafiki zao
8. Sio watu wenye kuzungumza sana kuhusu watu wengine na madhaifu yaw engine bali ni wenye kuzungumza zaidi kuhusu mawazo ya kujenga au mawazo ya kimaendeleo
9. Mara zote wana kiu ya kuona wengine wanafanikiwa, hata kama mafanikio hayo yatayazidi yale wao walionayo
10. Sio wachoyo katika kutoa taarifa au ujumbe wowote muhimu kwa mtu yeyote, maana wao hawana uchungu na mafanikio au ushindi wa mwingine
11. Ni watu wenye kuonyesha furaha wakati wote, sio wenye kununa, kuzira na kuwa na huzuni mara kwa mara
12. Ni watu wanaoweka malengo na kuongozwa na malengo katika maisha yao ya kila siku, sio wanaokurupuka kufanya mambo kwa hisia, misukumo au mashindano tu
13. Sio waoga wa mabadiliko, bali hutamani mabadiliko chanya na yenye kujenga na kuleta maendeleo, na kwahiyo mara zote kuyawezesha mabadiliko kutokea kwao na kwenye maisha ya wengine na sio kuyapinga
14. Kwao kujifunza ni tabia endelevu sio jambo linalotokea wakati wakiwa shuleni tu, wao huhesabu maisha ya kila siku ni kama shule
15. Kiu na msukumo wa maisha yao ya kila siku ni katika kusababisha mabadiliko, aidha mabadiliko kwao wao binafsi au kwa wale wanaowazunguka.
NIMEKUBAMBA
MAMBO KUMI YA KUFURAHISHA NA HUWEZI KUYAFANYA:
1. Huwezi kuosha Macho kwa Sabuni
2. Huwezi kuhesabu Nywele zako
3. Huwezi kupumua kwa Pua na huku umetoa Ulimi
4. Unajaribu kufanya namba 3
6. Umeona inawezekana, sanasana unakuwa Kama Jibwa
7. Unatabasamu kwa kuwa umejiona Mjinga!
8. Umeruka namba
9. Unahakikisha Kama kweli 5 haipo.
10. Unacheka kwa kuwa nimekubamba!
Shea na wenzako na wewe uwabambe! 😆😆😆😆😆
MUME MPENDA UGOMVI
**MUME MPENDA UGOMVI**
Kila siku akirudi nyumbani hutafuta vijisababu visivyo na msingi.........
Siku hiyo mke akajitahidi kuweka mazingira safi.
Sebuleni pakafagiliwa kufutwa na kupangwa vizuri,
Chumbani kila kitu safi,
Watoto wameogeshwa wanang'aa,
Mke kajipamba kama siku ya harusi.
Mume kuingia akaangaza huku na huko kila kitu poa,
Kukaa kwenye kochi...mara akafoka....
"Mama Abdallah! Mama Abdallah!"
Mke: Labeika Mume wangu!
Mume: Liko wapi lile vumbi lilokuwa hapa kwenye coffee table??
Mke: Si nimelifuta mume wangu kwani kuna nini
Mume: Kuna namba ya simu muhimu nilikuwa nimeandika juu yake!!
Mke: mmmmhh!! Baba Abdallah!!!
😂😂😂😂😂
HARAKATI ZA KUFUNGA KAMPAINI UTAYAONA HAYA USISHANGAE
1.Television ya taifa na zingine washirika kumuonesha mwalimu Nyerere mara nyingi zaidi ya siku za nyuma wakiweka hotuba zisizoponda chama tawala lakini zikikaa mrengo wa kukitetea haya yatafanyika kuelekea 14 October kwenye kumbukumbu ya mwalimu
2. Umeme kuwepo siku nzima na nchi nzima siku zifuatazo siku CCM itakapoenda Mwanza na mikoa mingine mikubwa ili watu waweze kuona na kusikia mikutano yao live nchi nzima lakini mgao utaendelea siku wapinzani wap wangu wakipita mikoa hiyo hiyo either wakiwa wametangulia au baadaye.
3. Kukamatwa kwa kiongozi mkubwa wa chama kimoja kwa kosa lililompeleka mbasha au babu seya kortini na kutangazwa sana na vyombo vya habari ikiwemo kuwaweka wazi waathirika wa tukio hilo litapotokea kesi itaisha baadae baada ya uchaguzi.
4. Kulazimishwa kwa kuombwa sana kwa mke wa kiongozi wa kitaifa anayeheshimika kutoa tamko siku ya kilele cha maadhimisho ya marehemu mumewe kwa hotuba fupi itakayoandaliwa au mahojiano yatakayoandaliwa kuonesha kwamba fulani sio chaguo na mengineyo.
5. Kukamatwa kwa watu watakaokuwa na Silaha za kivita wakiitwa"magaidi wenye mafunzo ya kikomandoo"ambao watasema wameletwa na chama kimoja cha siasa kwa shughuli maalumu .kumbuka hawatakuwa watanzania watatoka nchi inayosifika kwa magaidi afrika .
7. Kujitoa au kushawishiwa kujitoa kwa chama kimoja au kiongozi wake mkuu kwa madai ya kutotendewa haki na muungano wao.
8.Wagombea urais wawili au watatu kutangaza kumuunga mkoani mgombea wa chama kingine na Hii wataifanya hadharani siku ya kufunga kampeni kwa hicho chama.
9.Siku ya ufungaji wa kampeni tutashuhudia mwenyekiti wa chama kimoja wenye mamlaka ki nchi akimtuhumu waziwazi na kumtaja jina mgombea wa chama pinzani na washirika wake wakuu kuhusika na ufisadi uliotajwa sana tukio hilo litafanyika na kuoneshwa live na TV na redio nchi nzima na kupewa uzito kwenye magazeti yote kesho yake.
Lakini siku inayofuata ambayo chama tuhumiwa kitataka kujibu mapigo umeme utakatika nchi nzima so hawatakuwa live zaidi ya uwanjani pia magazeti ya siku ya uchaguzi yatawekewa oda ya jumla na tutayapata jioni au tusipate kabisa yatakuwa yameandika habari hizo za kufunga kampeni na majibu ya tuhuma kwa uwazi na vielelezo lakini itakuwa too late.
10. Uchaguzi utagubikwa na fujo kwa karatasi kuchelewa Vituoni, polisi kutumia nguvu kubwa,watu kuvaa tishet za vyama wasivyoshabikia na kufanya vurugu ila tishet hzo ni mpyaaaa.
Baadhi ya vituo watu hawatapiga kura uhesabu wa kura kielectonic utaleta utata mkubwa kwa kutofautiana na uhalisia wa jumla ya kura zote.
Kurudiwa kura sehemu mbalimbali kwa sababu mbalimbali.
Kukamatwa kwa wapiga kura mamluki au wanaotaka kutumika kupigia
MENGINE NITALETA BAADAYE USINIBISHIE KAA UTICK KILA KITAKACHOTOKEA KUTOKANA NA MUDA KAMA NI MDAU CHUKUA TAHADHARI
Subscribe to:
Posts (Atom)