Makumi ya maelfu ya watu kutoka kabila la Amharic wameshiriki katika maandamano dhidi ya Serikali nchini Ethiopia katika mji wa kaskazini wa Gondar.
Waandamanaji hao wameitaka serikali kubadilisha uamuzi wake wa kuanzisha wilaya chini ya usimamizi wa kabila la Tigray.
Serikali ya Ethiopia inasema kuwa zaidi ya watu 10 wameuawa wakati wa makabiliano na polisi kuhusu eneo linalozozaniwa katika majuma ya hivi karibuni.
No comments:
Post a Comment