Tuesday, October 25, 2016

Mabadiliko yanayokuathiri wewe mwajiriwa na Ajira yako


Kwa Tanzania sasa hivi kupoteza kazi yako ni rahisi sana. Unaweza kwenda kazini leo ukakuta umefukuzwa.

Teknolojia inabadilisha kila kitu. Baada ya muda mfupi unaweza kukuta kazi yako inafanywa na mashine.

Kumbuka Sikwambii haya kukutia hofu ni Ukweli ili ujiandae Lolote laweza kutokea.

Mambo uliyokua huyajui:-

• Hakuna Tajiri alieajiriwa,matajiri wote wanamiliki biashara zao wenyewe. Usifikiri kuwa tajiri kwa kupitia kwenye ajira.

•  Huwezi kua tajiri kwa kutegemea mshahara wako anza sasa kufikiria na kufanya, buni mfumo utakaokutengenezea kipato wakati upo kwenye ajira kipato hicho kikizidi mshahara na fanya mpango uache kazi.

•  Kama hujui ni kwamba boss wako hana mpango wa kubadili maisha yako furaha yake yeye ni aone unamfanyia kazi kwa bidii. Ukiumwa leo ukabaki nyumbani miezi mitatu ukirudi kazini utakuta nafasi yako imeshachukuliwa.

•  Haijalishi una elimu kubwa kiasi gani au ndogo kiasi gani mwajiriwa ni mwajiriwa tu wote wana hatari moja/wote wanamfanyia kazi mtu, ukifukuzwa kazi leo maisha yako lazima yatayumba.

•  Kilio kimoja cha kila mwajiriwa ni mishahara haikutani. Unaweza kubadili hali hiyo leo kwa kua na mfumo wako unakutengenezea pesa nje ya ajira.

•  Usipoteze muda kuomba uongezewe mshahara au upande cheo waza kumiliki biashara yako mwenyewe.

•  Mshahara ukiongezeka ujue utatakiwa ufanye kazi nyingi zaidi/uzalishe Zaidi, ukipanda cheo ujue na majukumu yatakua mengi Zaidi. Pesa utakayoongezewa huwezi kuifurahia tena.

•  Kwenye mfumo wako mwenyewe ni kwamba kuna wakati utakua haupo lakini pesa zinaendelea kutengenezwa.

•  Kama unafarijiwa na mafao utakayopata uzeeni piga mahesabu ni kiasi gani utapokea na uone jinsi gani unapoteza muda.

•  Mafao unayoyasubiria baada ya miaka 40 ya ajira ungeweze kutengeneza mara 50 yake na kwa muendelezo yaani hiyo miaka 40 ya ajira ni miaka 5 tu inaweza kukufanya wewe uanze kuishi maisha ya kipato kinacholingana na mafao yako.

•  Ajira yako haikulindi bali inakufanya uwe mtumwa unauza muda na nguvu zako kila siku kipato ambacho siku zote hakitakaa kikutoshe.

•  Sikwambii haya ili uache kazi leo lah! Anza kujitengenezea mfumo leo ili undoke hapo bila maumivu wala hofu yeyote.

•  Zipo biashara nyingi za kuanza ukiwa kwenye ajira lakini changamoto kubwa ni kwamba zitakukosa wewe kwasababu upo kwenye ajira hivyo ukuaji wake utakua kwenye hatari kubwa sana.

•  Lakini zipo biashara ambazo unaweza kutenga ule muda wako wa ziada baada ya ajira ukawa unaikuza biashara hii na ikakuletea mafanikio makubwa sana.

Inawezekana wewe hujawahi kufikiria kua tajiri au kumiliki mali nyingi biashara zako na kadhalika lakini kujiajiri au kuwa na kipato cha ziada ni kitu cha muhimu kwa maana unakua hutegemei mshahara peke yake. Lolote linaweza kutokea kipindi hiki.

Kuwa makini na jitengezee njia za kukisaidia kabla mabaya hayajakufikia.

Mifumo ipo,

Tafakari, Chukua hatua
Huku ukimtanguliza Mwenyezi Mungu mbele.

VISA VYA WANAWAKE NA KUPONEA KUFA CHUPUCHUPU

NINGEKUFA KWA AJILI YA  MWANAMKE!!

Leo nimepita kisimani nikamkuta dada mmmoja akifua. ,Nikamuuliza eti dada unavijua visa vya wanawake??

Akajibu kaka niache, nikakomaa anijibu...
Badala ya kujbu akaanza kupiga mayowe, na kelele za kuomba msaada.. hadi wananchi wenye mapanga, mawe na mishale wakaanza kuja, dada huyo alivyoona wanakuja akajmwagia maji mwili mzima. Nikajua leo ndio mwisho wangu nikajuta sana kutaka kujua kila kitu..

Wananchi walivyofika, wakamuulza, kuna nini? Akawajibu, nilidumbukia kwenye kisima na huyu kaka ndie amensaidia!!
Wakanipongeza sana sana kisha wakaondoka...

Yule dada  akaniambia, hivyo ndivyo visa vya mwanamke anaweza kukuua au kukulinda! So muheshmu mwanamke hata kinafiki, usijfanye jeuri!!!

*KUOLEWA NI NDOTO KUU YA KILA MWANAMKE ALIYEKAMILIKA ILA KAMA UNA TABIA HIZI UTAZEEKEA NYUMBANI*


*1. Tamaa ya utajiri* fedha na mali nyingi pasipo kutambua kuwa vitu hutafutwa, hapa wengi hupoteza nyota zao kwa kukataa wengi wenye kipato cha kawaida na kujirahisisha kwa wenye nazo ambao kwa bahati mbaya wengi wao sio waoaji bali ni wahuni tu na watu wa anasa na kula bata mjin.

*2. Dharau,* maringo, kiburi na mashauzi yaani we kila mtu akikusogelea na kujaribu kuzungumza na wewe unaanza kumpandisha na kumshusha kisha una msonya. Wengi huishia kukupotezea wakijua either umewadharau au tayari una mtu wako ndio maana nyodo nyingi.

*3. Husali* hakika lazima wahuni watapata nafasi kwako na kukuchezea mpaka uchakae kama mtumba wa uvira. MWENYEZI MUNGU ndo  anaetoa BARAKA ukimuomba hakika atakuepushia kuingia midomon mwa dubu na fisi wanaokuwa wakikuvizia na kuja kama MALAIKA. Atakupa ufahamu wa kuwatambua na kuwashtukia mapema.

*4. Kuvaa nguo za ajabu ajabu kama changudoa*
. Sijui ni nani aliyewaambia kuwa mkivaa hivyo mnapendeza! Unakuta binti unavaa kama mcheza show za Casino yaani ukipita nguo yaonyesha kila kitu ukiinama ndio balaa kabisa yaani kimin kinafunuka kila kitu nje nje kwa style hiyo nani atakupeleka kwao?

*5. Kujipaka marangi ya ajabu ajabu usoni kama mwali wa kibembe*
au kizaramo kwanza mnatutisha tu.

*6. Kupenda kujirahisisha au kujipendekeza pendekeza kwa wanaume,*
yani ukiguswa kidogo tu twende.

*7. Kuwa na picha karibia 500 Facebook,* Twitter nk halafu picha zenyewe hazieleweki yani zimepigwa katika mavazi au mapozi ya ajabu ajabu, mara umebinua makalio, mara tumbo, mara mdomo,

*8. Kila unachofanya basi unakimbilia kupost mfano kwenye Facebook* na kadhalika
nyinginezo hata ukienda haja basi lazima upost.

*9. Ni mtu wa maneno maneno*
yani we kila unachokiona unaongea na kuropoka ropoka tu hauna break! mwanamke gani?

*10. Huna mawazo ya malengo* endelevu yani we kwenye kichwa chako kumejaa umbea tu sijui leo Wema Sepetu amefanya nini? Sijui Kim, Lupita amefanya vile na upuuzi mwingine.

*11 Mizinga.*
Yani siku ya pili tu baada ya kukutongoza unaanza " honey nataka galaxy" Htc" Huawei" mara baby nimeona nguo nzuri mara ooh baby yaani njaa inauma'' , utasindikiza harusi za wenzio hadi upigwe alama..

Waswahili husema, "Kama mzuri, Olewa"

Jihadhari na tabia hizi.
_Maneno makali ila ujumbe umefika.

Monday, October 24, 2016

Wanawake kuchunguzwa majeraha


Dar es Salaam. Wanawake na wasichana wasiopungua 250,  Oktoba 29 watafanyiwa uchunguzi wa majeraha ya viungo kutokana na ulemavu na ngozi.

Uchunguzi huo utafanywa na Taasisi ya Huduma za Afya ya Aga Khan, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kushirikiana na shirika la kimataifa la WomenforWomen kutoka Marekani.

Meneja Miradi wa Aga Khan, Nasreen Hassanali amesema jana kuwa watakaobainika kuathirika zaidi na ulemavu wa viungo na ngozi uliotokana na majanga ya moto na ajali watafanyiwa upasuaji bure kurekebisha sehemu hizo.

Alisema kambi ya uchunguzi itafanyika katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa saba mchana itakayoongozwa na daktari bingwa, Edwin Mrema.

HEKIMA YA LEO


*MAISHA YANA VITU 7,*

*1:- Furaha.*
*2:- Karaha.*
*3:- Misukosuko.*
*4:- Majonzi.*
*5:- Migogoro.*
*6:- Mikasa.*
*7:- Chuki.*

*Haya yote husababishwa na viumbe hai kama mimi na wewe, ili kuyashinda haya yakupasa uwe na mambo 4.*

*1:- Subira.*
*2:- Uelewa.*
*3:- Uvumilivu.*
*4:- Msamaha.*

*Lakini katika maisha yako pendelea sana kuwa na mambo 4.*

*1:- Msimamo.*
*2:- Mkweli.*
*3:- Ujasiri.*
*4:- Imani.*

*Ila epuka sana mambo 5.*

*1:- Udanganyifu.*
*2:- Uchoyo.*
*3:- Ubinafsi.*
*4:- Wizi.*
*5:- Kufitinisha.*

*Kumbuka kumjali anaekujali hata kama yupo mbali nawe.*
*Mpende anaekupenda hata kama hana kitu jali utu kuliko kitu.*
*Ibada ndo Nuru yako Duniani na Akhera.*

*Yaarabbi tupe Mwisho Mwemaa!!!*

Tuesday, October 18, 2016

BABA NIFUNDISHE KUHUSU WANAWAKE


"Nikufundishe nini mwanangu kuhusu wanawake? Baba yako nimezeeka ghafla nikiwa na ufahamu mdogo na mwanangu umeshakua kiasi cha kuhitaji elimu hii adhimu, nikupe neno gani?, labda hivi,

1.KUHUSU TAMAA ZAO. -Mwanamke yeyote anaweza kukutamani kimapenzi isipokuwa Mama yako.

2. KUHUSU HULKA ZAO.
-Wanawake wote huonesha upendo wao waziwazi isipokuwa wale waliotendwa kabla.

3.KUHUSU KUACHANA.
-Mwanaume kumuacha mwanamke anayempenda ni kama simba kuacha kula swala, Mwanamke kumuacha mwanaume ni rahisi kama swala kumkimbia Simba mzee.

4.KUHUSU TABIA.
-Jihadhari na maneno ya vijiweni kwamba wanawake wote wako sawa kitabia. No, lakini kumbuka hakuna Mwanamke asie Mwanamke.

5. KUHUSU MPENZI WA ZAMANI.
-Kujaribu kumsahau mwanamke uliyewahi kumpenda ni kama kumkumbuka mtu usiyemjua. Ni ngumu.

6. KUHUSU KUOA.
-Muhimu kuoa, na ni ngumu sana Kumjua mke mwema kabla ya kuoa, ni waigizaji wazuri sana. Kumbuka maneno ya Albert. " Muhimu kuoa, ukipata mke mwema utakuwa na furaha, ukipata mke mwovu utakuwa mwanafalsafa.

7. KUHUSU USALITI.
-Vizuri kujiandaa kisaikolojia kusalitiwa, la usipojiandaa ama waweza kuua mtu au hata kujiua. ukiua mtu maisha yako yatakosa furaha siku zote, ukijiua mwenyewe, hao waliokusaliti wanaweza kuishi kwa furaha zaidi ya ulivyokuwa hai.

8.KUHUSU PESA NA MAPENZI.
-Mapenzi bila pesa yanapatikana kwa wingi sana huko mbinguni, hapa duniani ni ngumu mno, lakini usihofu sana, kuna makubaliano bila pesa. Omba mungu.

9. KUHUSU UONGO.
-Wahenga walisema Ukweli unauma, Na mimi nakuambia "Uongo unaua"

10. KUHUSU KUWAJUA WANAWAKE.
-Ewe mwanangu, kutaka kumjua mwanamke unahitaji miaka mingi ya kuishi kuliko idadi ya nywele zao. Usihangaike na vitabu, makala, majarida, filamu, nyimbo na hotuba za wanaofundisha mandhari za wanawake. Kuna kanuni moja tu ya kupenda, " ili ubaki salama katika kupenda sharti ujipende kwanza".

...Basi mwanangu hayo ndio machache naweza kukuhusia, na wewe una nafasi ya kujifunza zaidi na kufundisha kwa ufanisi zaidi kuliko Mimi...
Umependa elimu gan hapo??

Thursday, October 13, 2016

MODELING INSPIRATION


Kila kinacho fanyika ndani ya maisha yetu ya kila siku kinaongozwa na nia,utayari,kujiamini,kujituma na kujisimamia"

Haiwezi kuwa rahisi mtu kutimiza ndoto zako katika maisha juu ya kile unacho kitazamia kama wewe mwenyewe haupo tayari kuona ndoto zako zikifanikiwa katika hilo :

Huyu ni model anayeishi South Africa .Ni model mwenye Albinism :

Hata siku moja hakutaka kuishi kwa kuikubali hali yake ya udhaifu wa ngozi,jamii inavyo mchukulia na jinsi hali nzima ya muonekano wake wa mwili ilivyo (Albino) ILA tangu akiwa na umri mdogo alijiandalia njia na mazingira mazuri ya kuiaminisha jamii kuwa anaweza na nimfano wa kuigwa :

Siku zote aliishi kwa kuamini yeye ni mshindi na nibora zaidi katika kila anacho kifanya kutetea ndoto zake za maisha kupitia modeling HAKURUHUSU hata siku moja mawazo na mitazamo ya watu wanao mzunguka viweze kumkatisha tamaa na kujihisi hana tena thamani katika dunia ya kuishi maisha ya ndoto zake:

Daima alitia nia na kujituma zaidi katika kuutafuta ushindi wa mawazo,uhuru,mafanikio na imani ya kile alicho kuwa anakitamania na kukiamini kwa muda mrefu kama sehemu ya maisha yake (modeling)............................... Wakati anaanza safari yake ya matumaini katika kupigania ndoto zake ndani ya modeling alianza na neno "Ipo siku" na alivyo zidi kusogea mbele zaidi akasema tena "Nimefika lakini bado si sehemu nayo taka kuwa"....................................... Furaha yake na lengo lake kubwa ilikuwa ni siku moja kutambulika na kuheshimika  zaidi Africa na dunia kwa ujumla kama South Africa's First International Male Model with Albinism na kweli mpaka sasa furaha yake katika ndoto hizo imesha onekana nakuwa sehemu ya mfano wa kuigwa :

Tulio wengi katika kuishi maisha ya kufanikiwa ndani ya ndoto zetu tulizo jiwekea huwa tunashindwa kufanikiwa na kuonekana wenye kukataa tamaa kwa sababu ya kutokuwa na msimamo wa mawazo,nia,kujiamini,utayari,kuthubutu na kujitokeza............................................... Unacho takiwa kujua ni kwamba maamuzi ya nguvu za kufanikiwa katika kile unacho kiamini kama sehemu ya maisha yako "vipo juu yako"

Shirikisho la walemavu limemvaa Waziri wa Afya


SHIRIKISHO la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) limeitaka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee kuwatambua watu wenye ulemavu kama kundi linalostahili kupata msamaha katika ulipiaji wa gharama za huduma za afya

Ummy Mwalimu Wazira wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee
Hatua hii inakuja ikiwa ni siku nne tu tangu Ummy Mwalimu,  Waziri wa wizara hiyo kuyataja makundi matatu yanayostahili kupata msamaha wa gharama za matibabu kuwa ni; watoto, wazee na wanawake wajawazito pekee.

Ummy Nderiananga, Mwenyekiti wa Shivyawata amewambia wanahabari leo jijini Dar es Salaam kuwa taarifa ya waziri Ummy Mwalimu kutolitaja kundi la walemavu kama sehemu ya makundi yanayosahili msamaha wa gharama za matibabu imeibua mjadala wenye hisia tofauti hasa kwa watu wenye ulemavu.

“Shivyawata inamtaka Waziri Ummy Mwalimu kuhakikisha kwamba waraka wa afya wa mwaka 2012, unawafikia watoa huduma za afya wa serikali kwani watu wenye ulemavu tunakabiliana na changamoto ya kutakiwa kuonyesha utambulisho maalumu kutoka serikali za mitaa.

Walemavu hatustahili kuhurumiwa bali kuzingatiwa kwa haki yetu ya msingi ya kupata huduma za afya bure kama makundi mengine,” amesema.

Nderiananga ameitaka Wizara ya Afya kufanya maboresho ya waraka wa afya wa mwaka 2012 ili huduma ya tiba bila malipo kwa walemavu isiishie kwenye hospitali, vituo vya afya na zahanati, bali pia katika hospitali za rufaa.

“Lakini pia Shivyawata tunaitaka Wizara ya Afya kutoa bima maalum za afya kwa watu wenye ulemavu ili kuepuka udhalilishaji na urasimu katika kupata huduma hizo katika vituo vya afya, zahanati na hospitali zote,” amesema Nderiananga.

Wednesday, October 12, 2016

CHEKA KIDOGO

*mama mwenye nyumba anajipodoa anashinda saloon kujipodoa lakini house girl hata mafuta usoni hapaki lakini akipita na khanga yake moja tuu nyumba inatetemeka���������������������������� huu mchezo hautaki mekapu*

SOMA HISTORIA YA CHE” GUEVARA MWANAMAPINDUZI HATARI DUNIANI,ALIYEONGOZA MAPINDUZI NCHINI CUBA

49 YEARS AFTER HIS ASSASSINATION:CELEBRATING LIFE & TIMES OF CHE GUEVARA

Jina lake halisi:Dr.ERNESTO RAFAEL GUEVARA de La Serna
Aliyefariki tarehe kama ya leo:9/10/1967

Mahali alipofia:La Higuera,Valle Grande-Bolivia.
Mzaliwa wa mji wa Rozario-Argentina,aliyepata masomo yake ya Udaktari katika chuo kikuu cha Bunos Airea(University of Bunos Aires)
Akiwa amezaliwa ktk familia yenye kipato cha kati,kwa leo tungemuita “mtoto wa kishua” CHE
Akiwa amebakiza mwaka mmoja kabla ya kumaliza masomo yake ya Udaktari,alitumia likizo kusafiri kwa pikipiki (Motorcycle) akiwa na rafikiye ALBERTO GRANADO na kutembea katika mataifa mbalimbali ya Amerika kusini ikiwemo Peru,Guatemala na akiwa katika,Safari alishuhudua Umasikini uliokithiri,Maradhi na unyonyaji wa jamii kutoka kwa makampuni ya kibwanyenye yaliyowekeza katika Amerika kusini.Akiwa Guatemala alishuhudia kupinduliwa kwa Rais Mzalendo,JACOB ALBERZ aliyechaguliwa na wananchi akiwa amelenga kurudisha Ardhi iliyokua imeporwa na Kampuni ya Kimarekani;AMERICAN FRUIT COMPANY.

Rais JACOB ALBERZ alipinduliwa kwa mpango wa CIA waliolenga kulinda maslahi ya Kampuni AMERICAN FRUIT COMPANY
Kwa mujibu wa yeye mwenyewe CHE GUEVARA katika Memoir yake,anasema alitamani baada ya kumaliza Masomo yake ya Udaktari ajikite hasa katika utafiti,awe mtafiti(Researcher)
Lakini kile alichokishuhudia GUATEMALA,PERU nk.kilitosha kubadili mawazo kuona kuna haja ya kuwa Mwananapinduzi kukomboa jamii kubwa aliyotopea ktk Umasikini na Unyonyaji
Baada ya kuhitimu masomo yake ya Udaktari aliondoka Argentina kuelekea Mexico alikokutana na RAUL CASTRO na FIDEL CASTRO wakiwa uhamishoni baada ya jaribio la kuvamia kambi ya jeshi ya Moncada na kumpindua Dikteta Fulgencio Batista kushindikana ikiwa ni mwaka 1957
Wakitumia Boat kwa jina “GRANMA” kutoka MEXICO walisafiri hadi CUBA walipoanza mapambano ya kumuondoa Dikteta Kibaraka wa marekani Fulgencio Batista,vita iliyodumu kwa miaka miwili mpaka mwaka mpya mwaka 1959 walipofanikiwa kuingia HAVANA wakitokea Milima ya Sierra Maestra,Santiago de CUBA. walikopigana vita ya msituni kwa miaka miwili kupitia vugu vugu la Julai 26(Julai 26 movement) lilioaisisiwa mwaka 1953 wakati wa jaribio la kuvamia na kupora silaha ktk kambi ya Jeshi ya Moncada kufeli.

Mwaka mpya 1959 yaani 1/1/1959 FIDEL,RAUL,CHE na CAMILO waliingia Havana na kuhitimisha mapinduzi,huku wakishangiliwa na maelfu ya wa CUBA waliojitokeza kuwalaki wapambanaji mahiri wakombozi wa CUBA huku Dikteta kibaraka Fulgencio Batista akikimbilia Marekani
Baada ya mapinduzi CHE alipewa majukumu makuu matatu:Waziri wa Viwanda,Mkuu wa Idara ya Ulinzi na Mkuu wa Benki kuu aliyesaini sarafu ya CUBA. “Peso” kwa jina lake “CHE”
Baada ya Mapinduzi FIDEL alimtuma CHE GUEVARA Katika mataifa mbali mbali kuimarisha Urafiki alikwenda Ulaya,Urusi,Asia na Afrika katika mataifa ya Algeria,Guinea,Misri nk.
Baada ya Safari hii aligundua bado kuna Mataifa mengi hayajapata Uhuru na Vita ya ukombozi inaendelea kuanzia Afrika,Asia na Amerika kusini pia.
Baada ya kukamilisha Ziara hii ndefu aliporejea HAVANA aliandika barua na kujiuzulu vyeo vyake vyote serikalini ikiwa ni pamoja na Uraia wa CUBA aliupata baada ya mapinduzi ya mwaja 1959.
Katika Barua ya kujiuzulu aliyomwandikia FIDEL alimweleza haoni sababu ya kuwa na vyeo serikalini wakati bado kuna watu wanateseka ktk mataifa mbalimbali,alimoumba FIDEL na serikali imtunzie Mkewe ALEIDA MARCH na Wanawe Ernesto,Aleida,Rafael maana inawezekana wanaweza wasimuone tena.Barua hii ilisomwa ba FIDEL ktk mkutano wa Hadhara jijini HAVANA waCUBA walilia na kusikitika juu ya maamuzi ya CHE
CHE alielekea ZAIRE(DRC) ya sasa akipitia Tanganyika(Tanzania) akivuka Ziwa Tanganyika na wapiganaji wake kadhaa aliotoka nao CUBA.Wakati huo LAURENT KABILA akiwa msituni anapigana kumuondoa Dikteta MOBUTU SE SEKO.CHE alikatishwa tamaa na udhaifu wa wapiganaji walioongozwa na Laurent Kabila walijikita kwenye Ulevi,ngono na Uporaji wa madini,CHE alirejea Tanganyika akikaa kwa muda na hatimaye kuelekea Bolivia ambapo wapiganaji walikua wakipigana na serikali Dhalimu.
Huku CIA wakimfuatilia wakimtumia kibaraka wao raia wa Cuba aliyekimbia marekani baada ya Mapinduzi FELIX RODRIGUEZ.ambaye alihibitisha uwepo wa CHE Bolivia
“CHE” alikamatwa na jeshi la Bolivia kwa maelekezo ya CIA akafungiwa katika nyumba moja iliyoko ktk eneo la Shule ktk kijiji cha LA HIGUERA-Mji wa Valle Grande baada ya mapigano makali na kupigwa risasi mguuni hivo kushindwa kukimbia hatimaye kukamatwa,ambapo FELIX RODRIGUEZ alituma telegraph Washington akajibiwa CHE GHEVARA auawe
Saa sita mchana tarehe 9/10/1967 kijana mdogo mwenye cheo cha Sajenti aitwaye:MARIO TERAN akiwa amelewa aliingia ktk Chumba alichokua amefungwa “CHE” na Bunduki
CHE GUEVARA alilomuona alimwambia “NAJUA UMEKUJA KUNIUA,NIPIGE RISASI WE MUOGA ILA UJUE UNAUA MWANAUME” English; “I KNOW YOU COME TO KILL ME,SHOOT COWARD BUT YOU ARE GOING TO KILL A MAN”
Habari za kuuawa CHE GUEVARA zilisambaa ulimwengu mzima kukawa na maombolezo na maandamano maeneo mbalimbali ulimwenguni kupinga Mauaji yake.Mwili wa CHE ulikatwa viganja kwa ajili ya CIA Kujiridhisha km ni CHE GUEVARA aliyeuawa kwa vipimo vya DNA.
CHE alizikwa katika kaburi la siri ambalo halikujulikana mpaka mwaka 2007 wataalamu(Archeologist) walipogundua kaburi lake huko Valle-Grande,Bolivia,Mabaki ya mwili wake yalipelekwa CUBA kwa Ndege maalum na kuhifadhiwa katika jengo la Makumbusho la CHE GUEVARA(CHE GUEVARA Museleom)-Jijini HAVANA
Mtoto pekee wa CHE GUEVARA ambaye yuko hai leo ni Dr.ALEIDA GUEVARA,Daktari bingwa wa watoto(Pediatrician) aliyeachwa na Baba akiwa na mwaka mmoja,ambaye serikali ya CUBA ilihudumia familia ya CHE baada ya kifo chake
Huyo ndo CHE GUEVARA kwa kifupi ambaye T-shirt zake zinavaliwa sana,Picha yake ni mashuhuri sana ktk stika za magari,na maeneo mbalimbali Ulimwenguni
Ceremos Como CHE,yaani “Tutakua kama CHE“ ni kauli mbiu ambayo watoto wadogo wa shule za msingi Nchini CUBA hufunzwa na kutumiwa km salam:CEREMOS COMO CHE
Long Live COMMANDANTE
Viva La Revolucion
HASTA LA VICTORIA SIEMPRE…!!! Until Victory Forever
Patria O Muerte,Vencermos ……… Homeland or Death,We shall Overcome
VIVA Commandante CHE GUEVARA

Monday, October 3, 2016

True star Rukia

This is #truestar Rukia, the oldest resident of #Kabangacentre. Like many older persons, she has special needs. Even more so because she was born with albinism. 

At 58 she has not been able to shine her light onto the world .

For #international #day of #olderpersons we want to enohasize that, PWAs, whether children or full-grown adults, have the right to be themselves and live in freedom in their communities or wherever they choose to be!

From one of albinism society foundation found at kigoma @kabangastars  - letthemshine #kabangastars #kabanga #kigoma #kasulu #kabangacenter #beautifulplace #beautifulpeople #pwa #albinismawareness #internationalolderpersonsday #ngo #socialprojects #takeaction #inmyskiniwin #happymonday